Mount Moriah Ministry of God
Mount Moriah Ministry of God, Ni huduma ipatayo misingi katika NENO LA MUNGU, Ni huduma ya MAOMBI, lengo letu ni kuondowa watu walio tekwa nyara au kufungwa na shetani na kuwaleta kwa kambi ya Mungu kupitiya nguvu ya maombi na Neno la Mungu. Tunapatikana nchini kenya mjini kakuma, lengo la blogi hii nikuzidi kuifikisha injili kwa wenye uitaji. Unaweza ongeya nasi kwenye baruwa pepe E-mail: mountmoriahministry@gmail.com ao kwenye sim (+254)714-981-516, kwa maitaji ao pendekezo zaidi, ubarikiwe
Monday, June 12, 2023
Mega Gospel Concert
Saturday, December 24, 2022
BAPTISM, BEGINNING OF NEW JOURNEY
Glory to God,
We've fulfilled the mission
Which mission has been given to us by our Lord in the book of Matthew 28:13, our Christian's have made a big decision through commitment and passionately to follow Jesus Christ and to be baptized as prescribed in the Bible.
Baptism is the beginning of new journey in our Christian's lives, it is matter of decision.
May Almighty God gives you a heart which will enable you to have a right decision. God bless you
#MountMoriahAustralia
Sunday, December 18, 2022
Neema
Kiingilio: Waefeso 2:1-5
[1]Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
[2]ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;
[3]ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine.
[4]Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda;
[5]hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
Neema ni Nini?
Neema ni hali ya kupewa ao kuhesabiwa kitu bila kustahili.
Pst Faida
Wednesday, April 20, 2022
Maana ya ndoto kiroho,sehemu ya pili
Ujambo mpendwa katika Kristo Yesu, ninakuja tena kwa mara nyingine kukuleteya somo hii “MAANA YA NDOTO KIROHO” THE MEANING OF DREAM SPIRITUALLY, party 2
www.mountmoriahministry.blogspot.com
Na, MS. Guillain
Karibu tena kwa somo, Katika sehemu hii ya pili tunakwenda kuangalia mambo makuu mawili, ambayo ni;
Aina za NDOTO ni zipi?
Namna ya kutambua NDOTO tunazoota ni ipi?
Aina Za Ndoto na tofauti zake:
Ni muhimu sana kujifunza aina za ndoto kwasababu, hizo aina ndizo zitatuongoza namna ya kuzikabili. Zipo aina kuu MBILI za NDOTO;
Ndoto za KIMWILI
Ndoto za KIROHO
A) Ndoto Za Kimwili:
“Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.” Mhubiri 5:3
Hizi ndoto huitwa PUMZIKO LA MWILI. Baada ya mwili kufanya kazi sana haswa kwa kutumia ile milango mitano ya fahamu; macho, pua, ulimi, ngozi na masikio.
Usiku unapolala; ni MWILI ndiyo unaolala bali MOYO (Roho na Nafsi) zinakuwa zinaishi. Picha ya mambo uliyoyafanya kwa matendo au kwa kuyafikiria inajirudia katika NJOZI, nayo inakuwa inaitwa ndoto za kimwili. Kwa wale wanaongaliaga movie za kutisha utakuta usiku ukiwa umelala unaota ndoto nawe umo katika wakati wa vitisho kama ulivyoangalia kwenye movie
Au unakuta ulikuwa unafikiria jambo, unatumia nguvu nyingi katika kufikiria. Unajikuta usiku unaota ndoto inayotokana na mawazo yako. Lakini pia hizi ndoto zinaweza kukutokea kwasababu za kiafya au ukuaji wa mwili. Ukia mgonjwa mwili unakuwa na uchovu sana hivyo unapata usingizi mzito kama pumziko nako unakupelekea kupata ndoto. Katika hatua fulani za ukuaji mwanadamu anakuwa anaota ndoto mbalimbali kama kuokota fedha, kurukia bondeni, kutembea kenye kivuko kidogo sana majini nk.
Sifa yake kubwa ni kwamba unapoota hiyo ndoto; inakuwa haikusonineshi wala haina mguso wa ndani wowote… Tofauti na ndoto za KIROHO.
B) Ndoto Za Kiroho:
Ayubu 33:14-16 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani; Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,”
Ndoto za kiroho unapoziota, zinakuja kwa mguso wa ndani ya moyo wako. Unakuta ni ndoto ya kawaida sana ila unapoiota inaanza kukupa msononeko sana. Unakuta unaota ndoto alafu baada ya ndoto ikaanza kukutesa sana moyo mwako. Hiyo ndoto usiipuuze; bali ipokee na kuihoji
Tabia ya muhimu nyingine ya ndoto za kiroho ni kwamba zinakuwa na msisitizo ndani yake… Utaiota mara ya kwanza, na mara ya pili na hata zaidi ya hapo.
Lakini zipo aina MBILI za NDOTO hizi za KIROHO; Nazo ni muhimu sana kuzitofautisha.
Aina MBILI za NDOTO ZA KIROHO ni:-
Ndoto za MUNGU
Ndoto za SHETANI
Mwanzo 40:5-7 “Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika. Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo?”
Hawa jamaa wawili, Yusufu aliwakuta wakiwa WAMEFADHAIKA asubuhi…. Kisa tu ni kuota NDOTO.
Mwanzo 28:16-19 “Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua. Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.”
Yakobo akaogopa na akaondoka asubuhi na mapema sana.
Mwanzo 41:8 “Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo.”
Roho ya Farao ilifadhaika sana baada ya kuota ndoto. Farao pia aliota ndoto hata mara mbili na ndivyo ndoto za kiroho zilivyo, zinakuwa na mkazo ama za msisitizo. Biblia inasema, “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;” Ayubu 33:14-15.
Ndoto za Mungu zinaitwa mara pengine kama ndoto za ufalme mkuu wa mbinguni (ufalme wa nuru) na ndoto za shetani zinaitwa tena ndoto za ufalme wa kuzimu (ufalme wa giza)
SWALI LINAKUJA: Unawezaje kutofautisha NDOTO YA MUNGU na NDOTO YA SHETANI?
Ndoto za kuroho ni malango ya kiroho ya Mungu kusema nawe au shetani kusema nawe. Zina madhara makubwa sana kimwili na kiroho.
Ili uweze kuzifanyia kazi NDOTO, unapaswa KUZICHUNGUZA kwa umakini sana. Siyo ndoto zote zinamaana kiroho, zingine ni ndoto za kimwili tu ambazo hazina maana sana za kufanyiwa kazi.
Sasa, Je utazitofautishaje??? Na kuzitofautisha ni lazima ili kuweze kuzikabili ndoto.
Ndoto za kimwili unapaswa kuzipuuza na kuzitupilia mbali; ila ndoto za kiroho zinahitaji kufanyiwa kazi mara moja. Sasa; Nitazitofautishaje hizo ndoto?
NDOTO ZA KIROHO tumesema ni MALANGO (OPENING) ya KIROHO ambayo ulimwengu wa kiroho unatumia kuwasiliana nawe. Shetani anaweza kutumia ndoto kupandikiza vitu kwako ambavyo usipovingoa vinaweza kwamisha maisha yako.
“Ndipo huyo Elifazi, Mtemani, akajibu na kusema, Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu likasikia manong’ono yake. Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu. Hofu iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha mifupa yangu yote. Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na nywele za mwili wangu zilisimama. Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu; Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena. Ayubu 4:1, 12-16.
Hapa kuna vitu vinne; yaani kuna:-
WAZO liliingia ndani yake kwa NDOTO.
Katika MASIKIO iliingia SAUTI iliyoharibu usikivu wake.
HOFU ilimwingia.
Mifupa yake ikaanza kutetemeka.
Kumbuka IMANI ni kuwa na HAKIKA na mambo yatarajiwayo. Ni bayana ya mambo yasiyoonekana. IMANI chanzo chake ni KUSIKIA; na kusikia huja kwa NENO la Kristo.
Kupitia NDOTO ZA KIROHO Mungu anakuwa anasema nawe:-
Ili kukupa taarifa Fulani
Ili kukuonya kwa jambo Fulani
Ili kukupa tahadhari fulani
Pia ni kupitia NDOTO ZA KIROHO shetani anakuwa anasema nawe:-
Ili kukudhoofisha
Ili kukutesa
Ili kukutoa katika uwepo wa Mungu
Usiipuuzie ndoto unayoota maana inaweza tumika; kukuletea ujumbe wa Mungu, Maonyo au shetani anaweza pandikiza vitu. Mara nyingi shetani hatakuja na NDOTO tu, atakuja na ISHARA na utampokea kwa sababu ya ISHARA au MUUJIZA.
Na yeye ataleta na ujumbe na itakuwa ngumu sana kwako kukataa kwa sababu umeona ISHARA au MUUJIZA. Na lengo kubwa ni kuwa “uache kumfuata Mungu” na “kumpenda Mungu kutapoa” na “utapoteza hofu ya Mungu”
Shetani akifanikiwa katika hiyo dhamira yake kupitia NDOTO; Unapoteza kuambatana na Mungu. Unatopeteza kusikia Mungu anachosema na utaanza kupotea na utaanza kusikia neno la mtumishi zaidi bila kufuata neno la Mungu. Na wengi wamekwama hapo. Wapo watumishi wameacha kumtumikia Mungu kwa sababu waliota NDOTO na kuna vitu vilikuja na mbwembwe na wakidhani ni Mungu kumbe wala siyo MUNGU.
“Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye. Kumbukumbu la Torati 13:1-4
Ndoto inaweza tumika na shetani:-
Kupandikiza unabii wa uongo kwa kutumia ishara.
Wanapewa uwezo wa kushawishi watu wasimfuate Mungu katika Kristo Yesu.
NDOTO ZA MUNGU unaweza sana kuzitofautisha na NDOTO ZA SHETANI. Kama unaota ndoto inakupa VITISHO katika maisha yako ya kiroho ama kimwili; ujue kabisa umetoa nafasi kwa SHETANI kusema nawe.
Kama utaota ndoto inakupa MATUMAINI katika safari ya maisha haswa ya kiroho n ahata ya kimwili; ujue kabisa bila shaka ndani yake kwamba ni MUNGU amesema nawe.
Sasa kwasababu NDOTO ni malango ya ulimwengu wa roho; kupitia ndoto hizo za kiroho mambo unayoota yanakuja kuwa dhahiri; yanatokea. Ulimwengu wa kiroho una athiri sasna ulimwengu wa kimwili.
Lazima utatambua kuwa hii ndoto ni MBAYA na INATISHA… hivyo basi ni shetani ndiye anasema nawe… Maana yake umeacha malango wazi hata shetani akapenya kusema nawe.
Kwa maana hiyo; unaweza sana kutofautisha NDOTO ZA KIROHO kwamba ipi ni ndoto ya MUNGU ama ipi ni NDOTO ya shetani.
MAANA YA NDOTO KIROHO
Utangulizi wa somo:
Tunakwenda kujifunza somo linaloitwa “MAANA YA NDOTO KIROHO”. Hapa tunakwenda kujifunza ndoto kwa uchambuzi wa kukidhi wenye utukufu wa Roho mtakatifu kitu wazungu wanaita ONEROLOGY na kama wengi wanavyodhani, hatutakwenda kufasiri ndoto wala kujifunza ufasiri wa ndoto kitu wanaita ONEROCRITIC.
Marejeo Yetu:
Katika mafundisho yetu tutarejea sana katika kitabu kimoja tu BIBLIA na si vinginevyo / The only book to be our reference is Holy Bible.
SEHEMU YA KWANZA:
Katika sehemu ya kwanza ya somo letu tunakenda kuangalia mambo makuu mawili;
- Ndoto ni nini?
- Nini tofauti ya Ndoto na Maono?
Ndoto Ni Nini?
Katika Biblia yangu kuna neno NDOTO limeandikwa kama mara 68 hivi; kwenye Mwanzo pekee ipo mara 33 na kwenye kitabu cha Nabii Daniel mara 27 na kwa Agano Jipya naliona mara 8 pekee.
Wakati Biblia yangu imesheheni watumishi lukuki wa Mungu. Ni “watu wawili pekee” ndiyo ambao wametajwa katika “kufasiri NDOTO” ambao ni:
I. Yusufu na
II. Daniel
Maana ya ndoto;
Ndoto; ni hali inayotokea kwa mtu wakati anapokuwa katika usingizi mzito; hiyo hali ni udhihirisho wa kama hayupo usingizini na anafanya mambo fulani ya kawaida (yaliyo dhahiri) ama mambo yasiyo ya kawaidi (yasiyo dhahiri).
Mambo dhahiri; Haya mambo ni kama kuota ndoto ambamo muna kama watu, wanyama waliopo duniano na vitu vya kawaida vilivyopo duniani.
Mambo yasiyo dhahiri; Haya ni mambo ya ajabu, mara nyingi hayapo katika ulimwengu wa kawaida. Unaota nyoka anabadili umbo anakuwa na umbo la mpira wa miguu, unaota wanyama wa kutisha sana, ama viumbe au vitu ambavyo havipo kabisa katika ulimwengu huu wa mwili na nyama.
Kwa mara ya kwanza kabisa NDOTO imeandikwa kwenye Biblia katika Mwanzo 20:3.
“Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.” Mwanzo 20:3
Walioota ndoto katika BIBLIA;
Wapo watu kadhaa katika Biblia wanatajwa kwamba waliota NDOTO. Tutawaona watu 10 katika Agano la Kale na watu 3 katika Agano Jipya na tutajifunza kidogo kuhusu NDOTO zao.
1. Mfalme ABIMELEKI wa Gerari (Misri):
Mungu alimjia Abimeleki katika NDOTO usiku, siku ambapo alilala na mke wa Ibrahim, Sara… Mungu akamjia mmataifa (Gentile) kwa ndoto kinyume cha kawaida, kwasababu ya mtu wake mpendwa Ibrahim.
“Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.” Mwanzo 20:3
2. YAKOBO mwana wa Isaka;
Yakobo aliota NDOTO yake akiwa ameondoka nyumbani, akafika sehemu iitwa Luzu ambapo yeye akapabatiza jina la BETHELI kwa maana ya kuamini kwamba ndipo penye lango la Mbinguni. Aliota ndoto ya KUBARIKIWA KWAKE.
“Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.” Mwanzo 28:12
Yakobo akaota NDOTO nyingine tena akiwa katika machungo ya mifugo wa mjomba wake Laban. Pale walipokubaliana na Laban kuhusu mshahara wa kuchunga… Bado Yakobo aliota ndoto ya BARAKA.
“Ikawa, wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na madoadoa, na marakaraka.” Mwanzo 31:10
3. LABAN mjomba wa Yakobo, na mkwe.
Laban akiwa katika kumfuatia Yakobo baada ya kuondoka na miungu yake/vitu vya thamani na kwa kutoroka… Mungu alimjia huyu mtu wa mataifa tena kinyume na kawaida ila kwa manufaa ya mwanawe Yakobo. Alimwonya asije akamgusa Yakobo.
“Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.” Mwanzo 31:24
4. YUSUFU mwana wa Yakobo;
Yusufu akiwa na nduguze 12 kwa baba yao Yakobo; aliota ndoto ya ukuu wake juu ya watu wa kwao ikiwa ni pamoja na Baba na mama. Aliota ukuu wake na Kubarikiwa kwake.
“Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;” Mwanzo 37:5
“Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.” Mwanzo 37:9
5. MWOKAJI na MNYWESHAJI wa Ufalme wa Misri;
Hawa wawili wakiwa wamefungwa gereza moja pamoja na Yusufu; waliota ndoto katika usiku mmoja. Ni ndoto hizo ndizo zilizokusudiwa na Mungu kwaajili ya kumtoa kifungoni Yusufu na kuliinua jina lake.
“Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika.” Mwanzo 40:5-6
6. FARAO, Mfalme wa Misri:
Farao aliota ndoto, tena mara mbili katika usiku mmoja na akahitaji fasiri ya ndoto yake. Mungu alikusudia kumwotesha ndoto huyu mpagani kwaajili ya kuliinua jina la Yusufu na kutimiza ile ndoto ya Yusufu kuwa mkuu juu ya watu wa kwao.
“Ikawa, mwisho wa miaka miwili mizima, Farao akaota ndoto; na tazama, amesimama kando ya mto.” Mwanzo 41:1
“Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, masuke saba yalimea katika bua moja, makubwa, mema.” Mwanzo 41:5
“Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu.” Mwanzo 41:7
7. MMIDIANI na mwenzake;
Mungu aliikusudia ndoto ile ambayo mmidiani aliiota na kufasiriwa na mwenzake tena kwa ufunuo wa Mungu; lengo lake ni kumjaza imani Gideon na jeshi lake dogo, hakika Gideon alijaa imani kama makusudi ya NDOTO.
“Hata Gideoni alipofika, tazama, palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa akimhadithia mwenziwe ndoto, akasema, Tazama, naliota ndoto, na tazama, mkate wa shayiri ulianguka katika kambi ya Wamidiani, ukafika hata hema moja, ukaipiga hata ikaanguka, nao ukaipindua, hata ikalala chini. Mwenzake akamjibu akasema, Habari hii haikosi kuwa upanga wa Gideoni, mwana wa Yoashi, mtu wa Israeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote katika mkono wake. Ikawa, aliposikia habari ya ile ndoto, na kufasiriwa kwake, akasujudu; akarudi katika jeshi la Israeli akasema, Inukeni, kwa maana Bwana amelitia jeshi la Midiani mikononi mwenu.” Waamuzi 7:13-15
8. Mfalme SULEMANI wa Israel;
Kwa hakika wapendwa tunafahamu sana kuwa Suleiman alikuwa Mfalme mwenye hekima sana na tajiri aliyebarikiwa mno… Na tunajua alipewa fursa (favor) na akaomba kupewa HEKIMA. Fursa alikuwa amepewa “kwa njia ya NDOTO.” Nachelea kusema wengi wetu tumepoteza baraka nyingi kwasababu ya kupuuza ndoto ama kukosa ujasiri katika ndoto.
“Na huko Gibeoni Bwana akamtokea Sulemani katika ndoto ya usiku; Mungu akamwambia, Omba utakalo nikupe.” 1 Wafalme 3:5
9. Mfalme NEBUKADREZA wa Babeli;
Mfalme huyu mpagani aliota ndoto na akataka fasiri bila kuwaambia ndoto, alisema ameisahau; alipoona hawajui akataka kuwachinja… Ndipo Daniel jina lake likasimama. Hapa utagundua kuwa pamoja na maana nyingine, ila Mungu alikusudia kumwinua mwanae kwa njia hiyo. Mfalme aliota kuhusu ile “sanamu kubwa ya dhahabu safi inayong’aa sana”.
“Mfalme akawaambia, Nimeota ndoto, na roho yangu imefadhaika hata niijue tafsiri yake.” Danieli 2:3
10. DANIEL aliyeitwa Belteshaza;
Daniel aliota ndoto muhimu sana katika utumishi wake. Ndiyo hii ndoto iliyomfanyabkuitwa kwa jina NABII. Alioota ndoto nayo akaiandika ndiyo inayoweka mlango wa saba wa kitabu chake. Ni ndoto ya ufunuo wa nyakati zilizopo kuendelea hadi zijazo.
“Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danielii aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo.” Danieli 7:1
11. YUSUFU mume wa Maria;
Mungu alisema na Yusufu kwa njia ya NDOTO hata mara mbili. Alimwambia asimwache mchumba wake Maria kwaajili ya mimba. Na wakati mwingine akamwambia kuhusu kifo cha Herode na kwamba sasa warudi nyumbani kutoka uhamishoni.
“Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.” Mathayo 1:20
“Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,” Mathayo 2:19
12. MAMAJUSI wa Mashariki;
Hawa walipokwenda kwenye ufalme wa Herode aliwaambia mkimwona mfamle ajaye mrudi kunipasha habari nikamsabahi nikampe nami zawadi. Lakini Mungu akasema na hawa mamajusi kwa njia ya NDOTO kuhusu dhamira ya Herodi na kwamba waondoke kwa kupitia njia nyingine.
“Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.” Mathayo 2:12
“Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.” Mathayo 2:13
13. MKEWE Pilato;
Akiwa katika kutaka kutoa hukumu juu ya Yesu wa Nazareth, Pilato mkewe alimjia na kumuonya kutokunyoosha mkono wake juu ya Yesu kwasababu anakiri kupatabsana tabu usiku katika ndoto ya kwamba huyu Yesu kwamba ni mtu wa Haki na wala hana hatia. Nadhani utakumbuka ni Pilato ndiye aliyesema “mimi sioni hatia juu ya mtu huyu, nimenawa mikono yangu na damu yake isiwe juu yangu na nyumba yangu.”
“Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.” Mathayo 27:19
Tofauti Ya Ndoto Na Maono:
Zipo namna tatu za kuingia katika ulimwengu wa ROHO. Namna hizo ni kwa NDOTO na MAONO na MAOMBI. Kwa maana hiyo NDOTO na MAONO zote ni njia za kuingia katika ulimwengu wa ROHO. Lakini pia NDOTO ni ufunuo wa picha na matukio; ilhali MAONO pia.
Tofauti yao inakuja kwamba MAONO humpata mtu akiwa macho kabisa, ubongo wake ukiwa active wakati NDOTO inamtokea mtu akiwa katika usingizi mzito sana, mwili umepumzika na ubongo unafanya kazi.
Ukisoma Biblia utakuta karibu maeneo yote; ndoto na maono yametumiwa kwa namna moja. Unaweza kukuta ndoto inaitwa maono ama maono yakaitwa ndoto. Lakini pia haijaathiri maana halisi ya tofauti zao.
Sunday, April 17, 2022
Je, ni halili mkristo kuolewa ao kumuoa muislamu?
Jibu langu ni "Hapana", Lakini natumai utasoma vizuri maelezo yangu hapo chini ili kuelewa ni kwa nini nimesema "hapana".
»Itakuwa vyema tukitumia biblià kufahamu mkristo ni nani na muislamu ni nani.
»MKRISTO ni mtu aliyeokoka kwa kuamini kufa na kufufuka kwa Kristo na anamfuata Bwana Yesu. Tunaliona hili katika kitabu cha WARUMI 10:9 " Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua katika wafu; utaokoka".
»Tunapomuita Yesu kuwa ni Bwana yaani Bwana Yesu, tunamaanisha kuwa yeye ni kiongozi au mtawala wa maisha yetu tukifanya yote ayatakayo (MATHAYO 7:21).
»Kwa hiyo Mkristo hujibidisha kumpendeza Mungu, hata kama kuna muda ataonekana kushindwa(kuchelewa kuolewa), hapaswi kumkana Yesu. Kama ataziacha amri za Mungu, hatoweza kuingia katika ufalme wa Mungu pamoja na kwamba hapa duniani alijiita kuwa yeye ni Mkristo.
MUISLAMU NI NANI?
»Pamoja na maandiko mengi ya kiislamu kutakakufanana na ya Kikristo(kwa sababu walinakili), lakini imani ni tofauti na tofauti zake ni nyingi mno ukizichunguza kwa makini.
»Waislamu huamini Yesu kuwa ni nabii, hawaamini kuwa Yesu ni Mungu, wala hawaamini kuwa Yesu alifufuka. Hii ndio sababu ya Wakristo na Waislamu kutokuwa sambamba, kwa sababu wanaamini vitu tofauti kuhusu kiungo muhimu katika Ukristo yaani Yesu (WARUMI 10:9).
»Katika YOHANA 3:18 tunaona kuhusu Yesu " Amwaminiye yeye(Yesu) hahukumiwi(hana hatia); asiyemwamini(Yesu) amekwisha kuhukumiwa(ni mwenye hatia); kwa sababu hakuliamini jina pekee la mwana wa Mungu".
»Muislamu ni mwenye hatia, aliyehukumiwa tayari kwa sababu hamwamini Yesu.
»Tukisoma katika 2 WAKORINTHO 6:14-17 "Msifungiwe nira pamoja na wasioamini........yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?......." Mkristo hapaswi kuolewa na muislamu.
»Hata kama mwanamke(mkristo) amefiwa na mume yaani ni mjane, anaruhusiwa kuolewa na mtu yeyote amtakaye katika Bwana tu. 1 WAKORINTHO 7:39 " ....yu huru kuolewa na mtu yeyote amtakaye; katika Bwana tu".
»Hii ni amri ya Mungu na ni hekima pia, kwa sababu Mungu anatuambia mahusiano ya ndoa ni moja ya mambo yanayotusaidia kukua(kuimarika) kiroho na kuwa na nguvu za Kimungu na hayapaswi kutuzuia kukua kirohi.
»Kwa hiyo basi, wanamume wameamriwa kuwapenda wake zao na kuwafanya kuwa watakatifu(WAEFESO 5:25-33). Je, mwanamume wa kiislamu anaweza kufanya hivi hali yeye mwenyewe hamwamini Yesu? Jibu ni hapana hawezi badala yake ni kukuangusha kiroho na kukufanya uigeukie miungu ya kigeni ambayo ni chukizo kwa Mungu wetu.
»Tafuta kuwa karibu na Mungu, usikate tamaa kwa kuona umri umeenda wala huolewi; mwombe Mungu naye atakupa kwa wakati wake tena aonao kuwa wafaa.
»Je, unamfuata Yesu au unamwita Bwana, Bwana hali huyatendi yale asemayo? Je, unahakika kuwa ukifa unaingia mbinguni?
Jifunze kuusu Pasaka
»Neno "Pasaka" linatokana na neno la kiebrania "PESACH" kwa kiingereza ni lenye maana "PASS OVER" yaani "KUPITA JUU YA".
»Mwanzo wa Pasaka ulikuwa ni wakati wa nabii Musa (KUTOKA 12:14,17-18,21, KUTOKA 13:3-4; HESABU 9:21-30).
»Pasaka ni tendo la Bwana kupita juu ya nyumba za wana wa Israeli huko Misri, pale alipoiona damu ya mwanakondoo wa Pasaka katika vizingiti vya juu na miimo miwili ya milango yao alipita juu na kuacha kuwaharibu. Walioharibiwa walikuwa ni Wamisri ambao alama ya damu haikuonekana katika nyumba zao (KUTOKA 12:21-30).
»Mungu aliwaagiza wana wa Israeli kuikumbuka siku hii.
»Siku kuu hii ya Pasaka ilifanyika kuwa kumbukumbu kila mwaka katika mwezi wa Kiyahudi unaoitwa " NISAN" (NEHEMIA 2:1) au "ABIB" (KUTOKA 13:3-4). Siku kuu hii ilifanyikwa kwa juma moja yaani siku ya 14 hadi siku ya 21.(KUTOKA 12:14,17-18; HESABU 9:1-5).
»Mwezi wa "NISAN" au "ABIB" katika kalenda yetu ni kati ya mwezi "MARCHI" na "APRILI". Kuanza kwa mwezi ABIB kunategemeanana mwandamo wa mwezi . Ndiyo maana tarehe za siku kuu ya Pasaka hubadilika kila mwaka, Lakini huwa ni kati ya mwezi Marchi na Aprili.
»Katika kusherekea siku kuu hii walihitajika kuchinja wanyama wengi sana ili kupata damu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kama ondoleo la dhambi. Kwa wastani katika kipindi cha Pasaka walichinjwa wanyama 256,500 (laki mbili hamsini na sita elfu na mia tano).
»Katika kusherehekea Pasaka, Wayahudi walifanya mkutano mkubwa au konferensi ambapo walikusanyika pamoja na kula na kunywa na kuwa na muda mrefu wa kulisikia Neno la Mungu.
»Siku kuu hii iliendelea hadi katika kipindi cha Yesu Kristo. Yesu kristo mwenyewe alikuwa akienda kusherekea Pasaka(LUKA 2:41-52; YOHANA 2:13,23).
»Hiki kilikuwa ni kivuli cha Yesu Kristo kama mwanakondoo wa Pasaka aliyechinjwa msalabani.
»Yesu kristo alitolewa kusulubishwa wakati wa pasaka kama Pasaka wetu(YOHANA 18:39, 19:14-18; 1 WAKORINTHO 5:7). Kwa sababu hiyo, sasa hatuna haja ya kuchinja wanyamatena kama sadaka bali ni kumwamini Yesu ambaye ndiye sadaka yetu.
»Kila amwaminiye Yesu Kristo kwa Imani tu, damu ya Yesu hunyunyizwa juu yake na kuoshwa dhambi zote na kuwa salama(1 PETRO 1:2). Sasa hakuna haja tena ya kuchinja wanyama.Sasa tunaingia patakatifu pa Bwana(hekaluni) kwa damu ya Yesu(WAEBRANIA 10:19). Shetani ni Mharibu lakini hawezi kumharibu yeyote aliyenyunyiziwa damu ya Mwanakondoo (1 PETRO 1:2; UFUNUO 12:11).
»Kila asiyemwamini Yesu ghadhabu ya Mungu inamkalia, amekwisha hukumiwa (YOHANA 3:3,16-18). Kwa jinsi hiyo basi, ni busara mtu kusherehekea Pasaka pale tu ambapo amekwisha nyunyiziwa damu ya Yesu na kumshinda Shetani. Kinyume cha hapo, ni kufanya mchezo wa kuigiza(YOHANA 1:35-36, 10:10).
Thursday, April 14, 2022
Upendo unafaa kwa mkristo ao kwa kila mtu?
Ujambo mpendwa, ninakuja kukwambiya kwamba mda unaisha jaribu angalao kuwa na upendo kwa wale wanao kuudhi, kudharau, kuchukiya maana maandiko inasema wapendeni wanao wauzi.
Kristo ni UPENDO,na yeye ndiye sababu ya sisi kusamehewa dhambi, maana isinge likuwa upendo wa Mungu kwetu sisi, Nani angelisimama?
Wednesday, April 6, 2022
Kwa neno lako
Luc5:1-6
[1]Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,
[2]akaona vyombo viwili vimekaa kando ya ziwa, lakini wavuvi wametoka, wanaosha nyavu zao.
[3]Akaingia katika chombo kimoja, ndicho chake Simoni, akamtaka akipeleke mbali kidogo na pwani. Akaketi, akawafundisha makutano ali chomboni.
[4]Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki.
[5]Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.
[6]Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika;
Petro alikuwa bora sana katika urowaji lakini ujuzi haikumufanya apate samaki siku iyo. Inamaanisha kwamba kuna kitu ao utalaamu fulani petro aliitaji sana ili kupata samaki wengi. Nayo ilikuwa kukutana na Yesu Kristo.
Mtumbwi imekataa maji, sababu ilijuwa leo nisiku kubwa sipashwi kuvuwa ao kukaribisha mtu mwengine tofauti na Kristo. Kabla ya shuguli inabidi kwanza ni mpokeye yeye aliye Mkuu kuliko chochote. Ndiposa maandiko inasema kwamba
⬇️⬇️⬇️⬇️
Mimi Bwana ndiye nitakae kutanguliya mbele yako.
KUMBUKUMBU LA TORATI 31:8
Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha, usiogope wala usifadhaike.
Ndio mana baada ya mission being accomplished petro amerowa samaki wengi. Petro alikuwa under stress, machozi, usingisi maana alikuwa napenda kulala sana na nafikiri siku iyo petro akufika nhumbani sababu alikuwa ajapata kitu.
Kilicho mfanya petro stress imuishe ni kukubali kuachiliya chombo chake kiweze kuifikisha injili siku iyo. Amekubali wito na baada ya kukubali Jesus amejitukuza kwake.
⬇️⬇️⬇️⬇️
Mahali akili yako inaishiya ndiko ya Mungu inaanziya, usiogope maana Mungu yu pamoja nawe kila siku na kila wakati, haijalishi hali unayo ipitiya.
Kama uleshindwa kabizi Mungu shida, vikwazo na vyote avichukuwe yeye.
Yesu alikuwa na shabaa na petro sio mtumbwi, petro hakuwa na lolote lakufanya maana alikuwa tayari ameisha give up mapema. Na vile gisi mpango wa Mungu uko kila siku perfect God akunyamanza, alimwambiya petro baada tu ya kumaliza ebu egesha mtumbwi wako kule, pale.
Petro akasema KWA NENO LAKO NITAFANYA.
Sunday, April 3, 2022
Maisha ya ukristu wa leo
Ujambo mpendwa, natamani ku share nawewe jambo hili, ni kwa nini wakristu waleo wanapenda ao kutamani sana baraka lakini hawapendi kuhubiriwa kuusu dhambi? Unadhani shida nigani? Asante kwa mchango wako. uwe na wakati mwema. 🙏🙏🙏
Vifungo vya laana
Neno LAANA katika kamusi limetafsiriwa kama ukosefu wa radhi za mwenyezi Mungu, hasira ya Mungu. Au ni apizo atoalo mtu kwa mtu mwingine ili afikwe na ubaya, uovu, msiba au hasira ya Mungu. LAANI limetafsiliwa kama, shtakia kwa Mungu, au ombea uovu.
Zipo laana nyingi lakini leo ningependa kuzungumzia laana zifuatazo:-
Ukoo/familia:- laana zinazojiendeleza kwenye ukoo hutokana na matokeo ama matunda ya dhambi. Kwa mfano unakuta katika familia husika kuna wengine wana laana za magonjwa sugu kama kansa, kwenye hiyo hiyo familia wengine hawaolewi, wengine wameolewa lakini ndoa hazidumu, wengine hawapati mimba. Familia nyingine utakuta kuna vifo vya ghafla, wanaanza maisha na kufanikiwa na kuwa na mali na biashara kubwa au kazi lakini mwisho wao wanaishia kufilisika na kufa kwa mateso makali.Unatakiwa kuomba maombi ya rehema na toba na lazima utamke kilichofanyika na matokeo yake. Kwa sababu kila dhambi iliyofanyika ni kutokana na kuwa na miungu mingine. Dhambi inatokea pale mtu anapomwacha Mungu wa kweli na kusikiliza miungu mingine. Sasa unapokosa msaada wa Mungu wa kweli unapata misaada ya miungu inayokusababisha wewe kutenda kinyume na Mungu. “Usiwe na miungu mingine ila Mimi- Kumbukumbu la torati 5:7”
Laana za kulaaniwa na mtu mwingine:- Yawezekana ulikosana na rafiki yako ama mtu mwingine pengine mwalimu wako wa shule akakuchukia na kukulaani. Anaweza kukulaani kuwa na kamwe hutakaa uendelee kwa kila utakalofanya usifanikiwe.
Laana za kujilaani mwenyewe:- Kuna watu hawaridhiki na jinsi walivyo ama niseme viungo vya miili yao, yaani kwa ufupi hawajikubali ama kujiamini. Utakuta mtu analalamika na kusema “aah mimi kwa ufupi huu sidhani kama nitakaa nipate mwanamke mrefu atakaenipenda, ama mwingine atajilaani kwa kusema kamwe hawezi kuwa mtu wa kwanza darasani kwa sababu tu ya mtu fulani nyumbani kwao hajawahi kuwa” Siku zote maneno huumba na kujiumba, kwa maana hiyo yale uyatamkayo mdomoni kwako vivyo hivyo yanafanyika.
Laana ya vitu visivyoisha: Kuna watu wamelaaniwa kwa kila wakigusacho kisiendelee na matokeo yake hujikuta wameanzisha vitu mbali mbali bila hata kimojawapo kukamilika. Mfano mtu anataka kujenga lakini anaishia nusu na kuanza kitu kingine ambacho nacho hakifiki mbali. Nataka kuanzisha biashara ya nguo, atanunua sehemu ya kuuzia nguo lakini hakuna kitakachoendelea. Watu kama hawa ni wale wanaonena kwa midomo lakini hawatekelezi.
Laana ya kufanya tendo la ndoa na dada yako au kaka yako, baba yako au mama yako
Kuna mambo mengine sio rahisi hata kuelezea lakini yapo na yanafanyika mtu amelala na Dada yake, mwingine na kaka yake, laana ya Mungu imeagizwa juu yao “Kumb 27:22 Na alaaniwe alalaye na umbu lake, binti ya babaye au Binti ya mamae. Na watu wote waseme Amina”
Haya yote yanatokana na UPOFU wa mawazo. Akili ikifungwa mtu hawezi kufanya maamuzi yoyote. Pia akili ikifungwa mtu haoni ugumu wa dhambi. “2Wakorintho 3:14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi wakati lisomwapo Agano la kale, utaji uo huo wakaa, yaani haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo”. Soma pia Waefeso 4:18
NAVUNJAJE VIFUNGO?
Biblia inapozungumza habari ya watu waliofungwa wapate kufunguliwa, hii ina maana ya kuwa kuna watu wamefungwa chini ya utawala wa nguvu za giza katika ulimwengu wa Roho. Watu hawa wamefungwa kwenye magereza na Ibilisi.
Tutambue ya kuwa Yesu aliposema amekuja kutuokoa hii inamaanisha kwamba kuna mahali ambako tusingeweza kujikwamua wenyewe bila nguvu yake yeye mwenywe kuingia kati yetu.
Aliyahidhirisha haya kwenye kitabu cha nabii Isaya 61:1-2 Roho ya Bwana Mungu i juu yangu kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema, amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao”.
Vunja uhusiano wako na hiyo miungu pamoja na kazi zake na agano lililofanyika kati ya familia au ukoo wako na hiyo miungu. Kila unapotamka mwisho wake sema kwa sababu nimesamehewa. Ipo mistari mingi ya kuvunja maagano lakini mimi nitakupa kifungu hiki cha mstari katika kuvunja maagano na mapoozo ya aina yoyote. “Tena itakuwa katika siku hiyo mzigo wake utaondoka begani mwako na nira yake shingoni mwako, nayo nira itaharibiwa kwa sababu ya kutiwa mafuta” Isaya 10:27
Kifungu kingine ambacho waweza tumia ni kwa kutaja maneno haya wakati wa kuvunja vifungo ama laana “Bwana Yesu, nasimama mbele zako na katika ulimwengu wa roho, kujiachanisha nafsi yangu (Taja jina lako) na vifungo vya kuzimu kwa upande wa baba yangu na mama yangu kwa sababu nimesamehewa.” Endelea vivyo hivyo kwa kutaja, roho na mwili kwa kutumia maneno hayo hayo uponyaji hufanyika katika nafsi, mwili na roho.
Mtegemee Roho Mtakatifu kwa maana atakufundisha mengi ikiwemo kuomba na maagizo ya Yesu. Na kwa kufuata maagizo ya Yesu na kuenenda kwa roho hivyo vifungo vya nafsi vitakwisha. Soma Wagalatia 5:16-25, Luka 22:40-46. Kudumu katika maombi, kuenenda kiroho na kuepuka uovu ni muhimu kwa sababu kwa kufuata misingi hiyo ndipo unafunguliwa vifungo kwa kuombewa ama kwa nguvu inayotenda kazi ndani yako kupitioa roho mtakatifu. Lakini pia ni muhimu kujua ya kwamba sala ya toba pekee haitoshi kumfungua mtu kama ana vifungo na sio imani tu bali na juhudi binafsi ya mtu itasaidia katika kumuweka huru. Wapo watu wanaotaka kupokea miujiza bila ya kuwa na mabadiliko yoyote, ama bila kusoma neno la Mungu na kukua kiroho ama bila kuomba. Wao husubiria siku za maombi, ama mikesha ama makongamano ya maombi ili waombewe kisha baada ya hapo hawajishughulishi katika kukua kiimani.
Kuwa hodari katika Bwana ili upate ulinzi wa Mungu. Waefeso 6:10-11 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za shetani”
Maana ya kuwa hodari katika Bwana ni kukaa kwenye maombi, kusoma na kulishika neno lake liwe ndani yako, na kutaka kumjua yeye zaidi. Sikuzote Sali kwa bidii katika kupambana na muovu shetani ndo mana tunaambiwa vaeni silaha zote za Mungu ili kuweza kupingana na hila za muovu shetani.
Mbarikiwe na Mungu!
MS. Guillain
Mount Moriah Ministry of God, Mwinjilisti/Muandishi
Saturday, April 2, 2022
Jinsi ya kutambuwa manabii wa kweli
Katika somo hili nitaelezea jinsi ya kuwatambua manabii wa kweli wa Mungu kutokana na sifa walizokuwa nazo wakati wa Agano la Kale na Agano Jipya. Ni muhimu kila mkristo aliyeokoka aweze kupambanua (kutofautisha) na kutambua manabii wa kweli na manabii wa uongo. Manabii wa kweli walikuwa na sifa zifuatazo; 1.Walikuwa waaminifu. Hapa tutaangalia manabii watatu ambao ni Yesu, Musa na Samweli ambao walikuwa waaminifu katika mambo yote ya Mungu. Waebrania 3:1-2 “...Yesu aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama naye Musa alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu.” Katika andiko hili, Yesu amefananishwa na nabii Musa alivyokuwa mwaminifu. Mwingine ni Samweli, alipokuwa mzee aliwashuhudia wana wa Israel jinsi alivyokuwa mwaminifu tangu akiwa kijana. 1Samweli 12:2-4 “Basi sasa, angalieni, mfalme anakwenda mbele yenu; na mimi ni mzee, mwenye mvi; tena, tazameni, wana wangu wapo pamoja nanyi; nami nimekwenda mbele yenu toka ujana wangu hata leo. Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za BWANA, na mbele ya masihi wake, nalitwaa ng’ombe wa nani? Au nalitwaa punda wa nani? Au ni nani niliyemdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi. Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote.” 2.Walikuwa wakisema kile ambacho Mungu aliwaambia au kuwaonyesha bila kuongeza au kupunguza. 2Petro 1: 21 “Maana unabii haukutolewa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu”. 3.Walikuwa na bidii kuutafuta uso wa Mungu. Hapa nitawataja baadhi ya manabii ambao walikuwa wanaomba mbele za Mungu kwa bidii ambao ni; Yesu Kristo Bwana wetu, Eliya Mtishibi na Ana. Soma katika Biblia: Luka 22:41, Luka 2:36-37 na Yakobo 5:17-18. 4.Walikuwa wanyenyekevu na wenye hofu ya Mungu. 5.Walikuwa na huruma kwa ajili ya Taifa lao na kuliombea ili Mungu asilihukumu kutokana na makosa ambayo lilifanya. Hapa nitawataja baadhi yao ambao ni Musa na Samweli. Samweli 12:23 “Walakini mimi, hasha! Nisimtende BWANA dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka.” Kutoka 32:31-32 “Musa akarejea kwa BWANA akasema, Aa! Watu hawa wametenda dhambi kuu wamejifanyia miungu ya dhahabu. Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.” 6.Waliyoyatabiri yalitimia. Lakini kwa nyakati hizi za mwisho ni muhimu kwa kila mwamini kuwa makini na kufahamu ya kwamba siyo kila nabii asemaye unabii ukatimia na kutenda miujiza ni nabii wa kweli. Kumbukumbu 13:1-3 “Kukizuka katika yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia, akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikilize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto…” Kutokana na andiko hili hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba tunaweza kuwatambua manabii wanaopotosha kwa mambo yale wanayotuambia au kutuelekeza kinyume na neno la Mungu. Na ikiwa hawana matunda mazuri hao ni manabii wa uongo. Ndio maana imeandikwa; Mathayo 7:15-20 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa - mwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! watu huchukua zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.” Mfano wa mti mwema ni yule mtu anayeyafanya mapenzi ya Mungu (matakwa ya Mungu). Na mfano wa mti mwovu ni mtu asiyeyafanya mapenzi ya Mungu. 7.Unabii walioutoa ulilingana na neno la Mungu. Haukupigana na neno la Mungu mahali popote katika biblia. Mwamini anaweza kuutambua unabii kwa kutumia neno la Mungu. Lakini ni lazima kwanza ayafahamu maneno ya Mungu na kuyahifadhi moyoni. Wakolosai 3:16 "Na neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote…” Mtu akiwa na maneno ya Mungu kwa wingi moyoni anaweza kuyapima mambo yote ya Kiroho. Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo. Ni kwa njia zifuatazo; 1. Tunaweza kuwatambua au kuwapambanua kwa tabia zao ambazo haziendani na neno la Mungu na ziko dhahiri wala haziwezi kufichika. Tunaweza kuwatambua kwa kutumia neno la Mungu na tunda la Roho. Wagalatia 5:22-23 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” 2. Kuwatambua kwa mafundisho yao ya kibinadamu. Mafundisho yao wameyatunga hayaendani na neno la Mungu. Wanafundisha na kuhubiri kwa kutafsiri mistari ya biblia kinyume neno la Mungu. Kwa sababu hiyo wanakuwa wamewapotosha waamini katika njia ya Mungu. Hutumia mafundisho ya uzushi na uongo na kuyachanganya na maandiko ya neno la Mungu kana kwamba ni neno la Mungu. Kwa sababu hiyo huwapotosha wasiolijua neno la Mungu kwa ukamilifu. Ikiwa mwamini yuko makini na anayafahamu maandiko kwa ukamilifu ni lazima atagundua ya kwamba mafundisho wanayofundisha na kuyahubiri yanapingana na neno la Mungu katika biblia. Ndio maana imeandikwa tusiamini kila roho (kila nafsi) tuzijaribu kwanza. 1Yohana 4:1 “Wapenzi msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.” Mwalimu wa neno la Mungu. Ni muhimu kuwa makini anapotafsiri mistari ya neno la Mungu katika biblia, ni lazima ahakikishe inaendana na maandiko mengine katika biblia. asichokijua kwa usahihi asiwafundishe watu na kuwapotosha ili asije akahukumiwa. Imeandikwa; Ufunuo wa Yohana 22:18-19 “Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki. Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.” Kumbukumbu 4:2 “...neno niwaamurulo wala msilipunguze, mpate kuzishika amri za Bwana, Mungu wenu, niwaamuruzo.” Katika maandiko haya, Mungu ameonya tusije tukaongezea katika maneno yake ambayo yamekwisha kuandikwa. Kwa sababu hiyo hatupaswi kuchanganya neno la Mungu na mafundisho yetu ya kibinadamu. Pia ameonya tusiondoe wala kupunguza maneno ambayo yamekwisha kuandikwa kwenye kitabu chake. Jambo lingine limpasalo mtu kutambua ni kwamba maandiko yaliyomo katika biblia ni maneno ya unabii. Ufunuo wa Yohana 22:19 “Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.” Maneno ya unabii ni yale ambayo Mungu alisema na manabii wake kwa njia ya sauti, maono na ndoto, yakaandikwa katika biblia. Kwa sababu hiyo mtu anapofundisha neno la Mungu anakuwa anafundisha maneno ya unabii. Kwa kufanya hivyo si kwamba ametoa unabii. Unabii Unavyotokea Nabii anatoa unabii kwa yale ambayo Mungu amesema naye kwa njia ya sauti, maono na ndoto. Hesabu 12:6-8 “Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?” Tahadhari Kuhusu Kutoa Unabii. Ni muhimu kila mkristo aliyeokoka kuwa makini ili asije akahukumiwa kwa mambo haya yafuatayo; 1.Usitabiri uongo 2. Usipokee unabii wa uongo. Yeremia 14:14,16 “Ndipo BWANA akaniambia, Hao manabii wanatabiri uongo kwa jina langu mimi; mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo, na uaguzi, na neno la ubatili, na hadaa ya mioyo yao. Na watu hao, waliopewa unabii na wao, watatupwa nje katika njia kuu za Yerusalemu kwa sababu ya upanga na njaa; wala hawatakuwa na mtu wa kuwazika, wao na wake zao, na wana wao, na binti zao; maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.” Yeremia 23:31-32 “Tazama, mimi ni juu ya manabii, asema BWANA, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema, Tazama, mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA.” 3. Kuwa makini usiseme mambo ambayo Mungu hakusema na wewe kwa njia ya sauti, maoni na ndoto. Utakayoyasema hakikisha au thibitisha ni Mungu kweli amesema. Mungu anataka useme neno lake kwa uaminifu. Yeremia 23:28,31-32 “Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema BWANA. Tazama, mimi ni juu ya manabii, asema BWANA, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema, Tazama, mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi(...)