Mount Moriah Ministry of God
Mount Moriah Ministry of God, Ni huduma ipatayo misingi katika NENO LA MUNGU, Ni huduma ya MAOMBI, lengo letu ni kuondowa watu walio tekwa nyara au kufungwa na shetani na kuwaleta kwa kambi ya Mungu kupitiya nguvu ya maombi na Neno la Mungu. Tunapatikana nchini kenya mjini kakuma, lengo la blogi hii nikuzidi kuifikisha injili kwa wenye uitaji. Unaweza ongeya nasi kwenye baruwa pepe E-mail: mountmoriahministry@gmail.com ao kwenye sim (+254)714-981-516, kwa maitaji ao pendekezo zaidi, ubarikiwe
Friday, October 4, 2024
REASONS WHY WE SHOULD PRAISE THE LORD
“As for Me and My House, We Will Serve the Lord”
Friday, September 20, 2024
NGUVU YA MAOMBI
SIFA NA MAABUDU (New Generation)
matari na kinubi wamwimbie. 4 Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu. 5 Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao. 6 Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.” Tukiabudu Mungu hushuka. Uwepo wa Mungu ukiwepo mahali kila kitu utikiswa. Ndio maana Yesu alipofufuka makaburi yote yalipasuka na wafu wakatoka. Jifunze na tufanye kumsifu na kumwabudu Mungu kuwe sehemu ya maisha yetu. Kumsifu Mungu kunasababisha miujiza na nguvu ya Mungu kuonekana katika maisha yako.
Monday, June 12, 2023
Mega Gospel Concert
Saturday, December 24, 2022
BAPTISM, BEGINNING OF NEW JOURNEY
Glory to God,
We've fulfilled the mission
Which mission has been given to us by our Lord in the book of Matthew 28:13, our Christian's have made a big decision through commitment and passionately to follow Jesus Christ and to be baptized as prescribed in the Bible.
Baptism is the beginning of new journey in our Christian's lives, it is matter of decision.
May Almighty God gives you a heart which will enable you to have a right decision. God bless you
#MountMoriahAustralia
Sunday, December 18, 2022
Neema
Kiingilio: Waefeso 2:1-5
[1]Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
[2]ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;
[3]ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine.
[4]Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda;
[5]hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
Neema ni Nini?
Neema ni hali ya kupewa ao kuhesabiwa kitu bila kustahili.
Pst Faida
Wednesday, April 20, 2022
Maana ya ndoto kiroho,sehemu ya pili
Ujambo mpendwa katika Kristo Yesu, ninakuja tena kwa mara nyingine kukuleteya somo hii “MAANA YA NDOTO KIROHO” THE MEANING OF DREAM SPIRITUALLY, party 2
www.mountmoriahministry.blogspot.com
Na, MS. Guillain
Karibu tena kwa somo, Katika sehemu hii ya pili tunakwenda kuangalia mambo makuu mawili, ambayo ni;
Aina za NDOTO ni zipi?
Namna ya kutambua NDOTO tunazoota ni ipi?
Aina Za Ndoto na tofauti zake:
Ni muhimu sana kujifunza aina za ndoto kwasababu, hizo aina ndizo zitatuongoza namna ya kuzikabili. Zipo aina kuu MBILI za NDOTO;
Ndoto za KIMWILI
Ndoto za KIROHO
A) Ndoto Za Kimwili:
“Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.” Mhubiri 5:3
Hizi ndoto huitwa PUMZIKO LA MWILI. Baada ya mwili kufanya kazi sana haswa kwa kutumia ile milango mitano ya fahamu; macho, pua, ulimi, ngozi na masikio.
Usiku unapolala; ni MWILI ndiyo unaolala bali MOYO (Roho na Nafsi) zinakuwa zinaishi. Picha ya mambo uliyoyafanya kwa matendo au kwa kuyafikiria inajirudia katika NJOZI, nayo inakuwa inaitwa ndoto za kimwili. Kwa wale wanaongaliaga movie za kutisha utakuta usiku ukiwa umelala unaota ndoto nawe umo katika wakati wa vitisho kama ulivyoangalia kwenye movie
Au unakuta ulikuwa unafikiria jambo, unatumia nguvu nyingi katika kufikiria. Unajikuta usiku unaota ndoto inayotokana na mawazo yako. Lakini pia hizi ndoto zinaweza kukutokea kwasababu za kiafya au ukuaji wa mwili. Ukia mgonjwa mwili unakuwa na uchovu sana hivyo unapata usingizi mzito kama pumziko nako unakupelekea kupata ndoto. Katika hatua fulani za ukuaji mwanadamu anakuwa anaota ndoto mbalimbali kama kuokota fedha, kurukia bondeni, kutembea kenye kivuko kidogo sana majini nk.
Sifa yake kubwa ni kwamba unapoota hiyo ndoto; inakuwa haikusonineshi wala haina mguso wa ndani wowote… Tofauti na ndoto za KIROHO.
B) Ndoto Za Kiroho:
Ayubu 33:14-16 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani; Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,”
Ndoto za kiroho unapoziota, zinakuja kwa mguso wa ndani ya moyo wako. Unakuta ni ndoto ya kawaida sana ila unapoiota inaanza kukupa msononeko sana. Unakuta unaota ndoto alafu baada ya ndoto ikaanza kukutesa sana moyo mwako. Hiyo ndoto usiipuuze; bali ipokee na kuihoji
Tabia ya muhimu nyingine ya ndoto za kiroho ni kwamba zinakuwa na msisitizo ndani yake… Utaiota mara ya kwanza, na mara ya pili na hata zaidi ya hapo.
Lakini zipo aina MBILI za NDOTO hizi za KIROHO; Nazo ni muhimu sana kuzitofautisha.
Aina MBILI za NDOTO ZA KIROHO ni:-
Ndoto za MUNGU
Ndoto za SHETANI
Mwanzo 40:5-7 “Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika. Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo?”
Hawa jamaa wawili, Yusufu aliwakuta wakiwa WAMEFADHAIKA asubuhi…. Kisa tu ni kuota NDOTO.
Mwanzo 28:16-19 “Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua. Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. Akaita jina la mahali pale Betheli; lakini jina la mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.”
Yakobo akaogopa na akaondoka asubuhi na mapema sana.
Mwanzo 41:8 “Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo.”
Roho ya Farao ilifadhaika sana baada ya kuota ndoto. Farao pia aliota ndoto hata mara mbili na ndivyo ndoto za kiroho zilivyo, zinakuwa na mkazo ama za msisitizo. Biblia inasema, “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;” Ayubu 33:14-15.
Ndoto za Mungu zinaitwa mara pengine kama ndoto za ufalme mkuu wa mbinguni (ufalme wa nuru) na ndoto za shetani zinaitwa tena ndoto za ufalme wa kuzimu (ufalme wa giza)
SWALI LINAKUJA: Unawezaje kutofautisha NDOTO YA MUNGU na NDOTO YA SHETANI?
Ndoto za kuroho ni malango ya kiroho ya Mungu kusema nawe au shetani kusema nawe. Zina madhara makubwa sana kimwili na kiroho.
Ili uweze kuzifanyia kazi NDOTO, unapaswa KUZICHUNGUZA kwa umakini sana. Siyo ndoto zote zinamaana kiroho, zingine ni ndoto za kimwili tu ambazo hazina maana sana za kufanyiwa kazi.
Sasa, Je utazitofautishaje??? Na kuzitofautisha ni lazima ili kuweze kuzikabili ndoto.
Ndoto za kimwili unapaswa kuzipuuza na kuzitupilia mbali; ila ndoto za kiroho zinahitaji kufanyiwa kazi mara moja. Sasa; Nitazitofautishaje hizo ndoto?
NDOTO ZA KIROHO tumesema ni MALANGO (OPENING) ya KIROHO ambayo ulimwengu wa kiroho unatumia kuwasiliana nawe. Shetani anaweza kutumia ndoto kupandikiza vitu kwako ambavyo usipovingoa vinaweza kwamisha maisha yako.
“Ndipo huyo Elifazi, Mtemani, akajibu na kusema, Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu likasikia manong’ono yake. Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu. Hofu iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha mifupa yangu yote. Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na nywele za mwili wangu zilisimama. Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu; Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena. Ayubu 4:1, 12-16.
Hapa kuna vitu vinne; yaani kuna:-
WAZO liliingia ndani yake kwa NDOTO.
Katika MASIKIO iliingia SAUTI iliyoharibu usikivu wake.
HOFU ilimwingia.
Mifupa yake ikaanza kutetemeka.
Kumbuka IMANI ni kuwa na HAKIKA na mambo yatarajiwayo. Ni bayana ya mambo yasiyoonekana. IMANI chanzo chake ni KUSIKIA; na kusikia huja kwa NENO la Kristo.
Kupitia NDOTO ZA KIROHO Mungu anakuwa anasema nawe:-
Ili kukupa taarifa Fulani
Ili kukuonya kwa jambo Fulani
Ili kukupa tahadhari fulani
Pia ni kupitia NDOTO ZA KIROHO shetani anakuwa anasema nawe:-
Ili kukudhoofisha
Ili kukutesa
Ili kukutoa katika uwepo wa Mungu
Usiipuuzie ndoto unayoota maana inaweza tumika; kukuletea ujumbe wa Mungu, Maonyo au shetani anaweza pandikiza vitu. Mara nyingi shetani hatakuja na NDOTO tu, atakuja na ISHARA na utampokea kwa sababu ya ISHARA au MUUJIZA.
Na yeye ataleta na ujumbe na itakuwa ngumu sana kwako kukataa kwa sababu umeona ISHARA au MUUJIZA. Na lengo kubwa ni kuwa “uache kumfuata Mungu” na “kumpenda Mungu kutapoa” na “utapoteza hofu ya Mungu”
Shetani akifanikiwa katika hiyo dhamira yake kupitia NDOTO; Unapoteza kuambatana na Mungu. Unatopeteza kusikia Mungu anachosema na utaanza kupotea na utaanza kusikia neno la mtumishi zaidi bila kufuata neno la Mungu. Na wengi wamekwama hapo. Wapo watumishi wameacha kumtumikia Mungu kwa sababu waliota NDOTO na kuna vitu vilikuja na mbwembwe na wakidhani ni Mungu kumbe wala siyo MUNGU.
“Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye. Kumbukumbu la Torati 13:1-4
Ndoto inaweza tumika na shetani:-
Kupandikiza unabii wa uongo kwa kutumia ishara.
Wanapewa uwezo wa kushawishi watu wasimfuate Mungu katika Kristo Yesu.
NDOTO ZA MUNGU unaweza sana kuzitofautisha na NDOTO ZA SHETANI. Kama unaota ndoto inakupa VITISHO katika maisha yako ya kiroho ama kimwili; ujue kabisa umetoa nafasi kwa SHETANI kusema nawe.
Kama utaota ndoto inakupa MATUMAINI katika safari ya maisha haswa ya kiroho n ahata ya kimwili; ujue kabisa bila shaka ndani yake kwamba ni MUNGU amesema nawe.
Sasa kwasababu NDOTO ni malango ya ulimwengu wa roho; kupitia ndoto hizo za kiroho mambo unayoota yanakuja kuwa dhahiri; yanatokea. Ulimwengu wa kiroho una athiri sasna ulimwengu wa kimwili.
Lazima utatambua kuwa hii ndoto ni MBAYA na INATISHA… hivyo basi ni shetani ndiye anasema nawe… Maana yake umeacha malango wazi hata shetani akapenya kusema nawe.
Kwa maana hiyo; unaweza sana kutofautisha NDOTO ZA KIROHO kwamba ipi ni ndoto ya MUNGU ama ipi ni NDOTO ya shetani.
MAANA YA NDOTO KIROHO
Utangulizi wa somo:
Tunakwenda kujifunza somo linaloitwa “MAANA YA NDOTO KIROHO”. Hapa tunakwenda kujifunza ndoto kwa uchambuzi wa kukidhi wenye utukufu wa Roho mtakatifu kitu wazungu wanaita ONEROLOGY na kama wengi wanavyodhani, hatutakwenda kufasiri ndoto wala kujifunza ufasiri wa ndoto kitu wanaita ONEROCRITIC.
Marejeo Yetu:
Katika mafundisho yetu tutarejea sana katika kitabu kimoja tu BIBLIA na si vinginevyo / The only book to be our reference is Holy Bible.
SEHEMU YA KWANZA:
Katika sehemu ya kwanza ya somo letu tunakenda kuangalia mambo makuu mawili;
- Ndoto ni nini?
- Nini tofauti ya Ndoto na Maono?
Ndoto Ni Nini?
Katika Biblia yangu kuna neno NDOTO limeandikwa kama mara 68 hivi; kwenye Mwanzo pekee ipo mara 33 na kwenye kitabu cha Nabii Daniel mara 27 na kwa Agano Jipya naliona mara 8 pekee.
Wakati Biblia yangu imesheheni watumishi lukuki wa Mungu. Ni “watu wawili pekee” ndiyo ambao wametajwa katika “kufasiri NDOTO” ambao ni:
I. Yusufu na
II. Daniel
Maana ya ndoto;
Ndoto; ni hali inayotokea kwa mtu wakati anapokuwa katika usingizi mzito; hiyo hali ni udhihirisho wa kama hayupo usingizini na anafanya mambo fulani ya kawaida (yaliyo dhahiri) ama mambo yasiyo ya kawaidi (yasiyo dhahiri).
Mambo dhahiri; Haya mambo ni kama kuota ndoto ambamo muna kama watu, wanyama waliopo duniano na vitu vya kawaida vilivyopo duniani.
Mambo yasiyo dhahiri; Haya ni mambo ya ajabu, mara nyingi hayapo katika ulimwengu wa kawaida. Unaota nyoka anabadili umbo anakuwa na umbo la mpira wa miguu, unaota wanyama wa kutisha sana, ama viumbe au vitu ambavyo havipo kabisa katika ulimwengu huu wa mwili na nyama.
Kwa mara ya kwanza kabisa NDOTO imeandikwa kwenye Biblia katika Mwanzo 20:3.
“Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.” Mwanzo 20:3
Walioota ndoto katika BIBLIA;
Wapo watu kadhaa katika Biblia wanatajwa kwamba waliota NDOTO. Tutawaona watu 10 katika Agano la Kale na watu 3 katika Agano Jipya na tutajifunza kidogo kuhusu NDOTO zao.
1. Mfalme ABIMELEKI wa Gerari (Misri):
Mungu alimjia Abimeleki katika NDOTO usiku, siku ambapo alilala na mke wa Ibrahim, Sara… Mungu akamjia mmataifa (Gentile) kwa ndoto kinyume cha kawaida, kwasababu ya mtu wake mpendwa Ibrahim.
“Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, Umekuwa mfu wewe kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu.” Mwanzo 20:3
2. YAKOBO mwana wa Isaka;
Yakobo aliota NDOTO yake akiwa ameondoka nyumbani, akafika sehemu iitwa Luzu ambapo yeye akapabatiza jina la BETHELI kwa maana ya kuamini kwamba ndipo penye lango la Mbinguni. Aliota ndoto ya KUBARIKIWA KWAKE.
“Akaota ndoto; na tazama, ngazi imesimamishwa juu ya nchi, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake.” Mwanzo 28:12
Yakobo akaota NDOTO nyingine tena akiwa katika machungo ya mifugo wa mjomba wake Laban. Pale walipokubaliana na Laban kuhusu mshahara wa kuchunga… Bado Yakobo aliota ndoto ya BARAKA.
“Ikawa, wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na madoadoa, na marakaraka.” Mwanzo 31:10
3. LABAN mjomba wa Yakobo, na mkwe.
Laban akiwa katika kumfuatia Yakobo baada ya kuondoka na miungu yake/vitu vya thamani na kwa kutoroka… Mungu alimjia huyu mtu wa mataifa tena kinyume na kawaida ila kwa manufaa ya mwanawe Yakobo. Alimwonya asije akamgusa Yakobo.
“Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.” Mwanzo 31:24
4. YUSUFU mwana wa Yakobo;
Yusufu akiwa na nduguze 12 kwa baba yao Yakobo; aliota ndoto ya ukuu wake juu ya watu wa kwao ikiwa ni pamoja na Baba na mama. Aliota ukuu wake na Kubarikiwa kwake.
“Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia;” Mwanzo 37:5
“Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.” Mwanzo 37:9
5. MWOKAJI na MNYWESHAJI wa Ufalme wa Misri;
Hawa wawili wakiwa wamefungwa gereza moja pamoja na Yusufu; waliota ndoto katika usiku mmoja. Ni ndoto hizo ndizo zilizokusudiwa na Mungu kwaajili ya kumtoa kifungoni Yusufu na kuliinua jina lake.
“Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika.” Mwanzo 40:5-6
6. FARAO, Mfalme wa Misri:
Farao aliota ndoto, tena mara mbili katika usiku mmoja na akahitaji fasiri ya ndoto yake. Mungu alikusudia kumwotesha ndoto huyu mpagani kwaajili ya kuliinua jina la Yusufu na kutimiza ile ndoto ya Yusufu kuwa mkuu juu ya watu wa kwao.
“Ikawa, mwisho wa miaka miwili mizima, Farao akaota ndoto; na tazama, amesimama kando ya mto.” Mwanzo 41:1
“Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, masuke saba yalimea katika bua moja, makubwa, mema.” Mwanzo 41:5
“Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu.” Mwanzo 41:7
7. MMIDIANI na mwenzake;
Mungu aliikusudia ndoto ile ambayo mmidiani aliiota na kufasiriwa na mwenzake tena kwa ufunuo wa Mungu; lengo lake ni kumjaza imani Gideon na jeshi lake dogo, hakika Gideon alijaa imani kama makusudi ya NDOTO.
“Hata Gideoni alipofika, tazama, palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa akimhadithia mwenziwe ndoto, akasema, Tazama, naliota ndoto, na tazama, mkate wa shayiri ulianguka katika kambi ya Wamidiani, ukafika hata hema moja, ukaipiga hata ikaanguka, nao ukaipindua, hata ikalala chini. Mwenzake akamjibu akasema, Habari hii haikosi kuwa upanga wa Gideoni, mwana wa Yoashi, mtu wa Israeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote katika mkono wake. Ikawa, aliposikia habari ya ile ndoto, na kufasiriwa kwake, akasujudu; akarudi katika jeshi la Israeli akasema, Inukeni, kwa maana Bwana amelitia jeshi la Midiani mikononi mwenu.” Waamuzi 7:13-15
8. Mfalme SULEMANI wa Israel;
Kwa hakika wapendwa tunafahamu sana kuwa Suleiman alikuwa Mfalme mwenye hekima sana na tajiri aliyebarikiwa mno… Na tunajua alipewa fursa (favor) na akaomba kupewa HEKIMA. Fursa alikuwa amepewa “kwa njia ya NDOTO.” Nachelea kusema wengi wetu tumepoteza baraka nyingi kwasababu ya kupuuza ndoto ama kukosa ujasiri katika ndoto.
“Na huko Gibeoni Bwana akamtokea Sulemani katika ndoto ya usiku; Mungu akamwambia, Omba utakalo nikupe.” 1 Wafalme 3:5
9. Mfalme NEBUKADREZA wa Babeli;
Mfalme huyu mpagani aliota ndoto na akataka fasiri bila kuwaambia ndoto, alisema ameisahau; alipoona hawajui akataka kuwachinja… Ndipo Daniel jina lake likasimama. Hapa utagundua kuwa pamoja na maana nyingine, ila Mungu alikusudia kumwinua mwanae kwa njia hiyo. Mfalme aliota kuhusu ile “sanamu kubwa ya dhahabu safi inayong’aa sana”.
“Mfalme akawaambia, Nimeota ndoto, na roho yangu imefadhaika hata niijue tafsiri yake.” Danieli 2:3
10. DANIEL aliyeitwa Belteshaza;
Daniel aliota ndoto muhimu sana katika utumishi wake. Ndiyo hii ndoto iliyomfanyabkuitwa kwa jina NABII. Alioota ndoto nayo akaiandika ndiyo inayoweka mlango wa saba wa kitabu chake. Ni ndoto ya ufunuo wa nyakati zilizopo kuendelea hadi zijazo.
“Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danielii aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo.” Danieli 7:1
11. YUSUFU mume wa Maria;
Mungu alisema na Yusufu kwa njia ya NDOTO hata mara mbili. Alimwambia asimwache mchumba wake Maria kwaajili ya mimba. Na wakati mwingine akamwambia kuhusu kifo cha Herode na kwamba sasa warudi nyumbani kutoka uhamishoni.
“Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.” Mathayo 1:20
“Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,” Mathayo 2:19
12. MAMAJUSI wa Mashariki;
Hawa walipokwenda kwenye ufalme wa Herode aliwaambia mkimwona mfamle ajaye mrudi kunipasha habari nikamsabahi nikampe nami zawadi. Lakini Mungu akasema na hawa mamajusi kwa njia ya NDOTO kuhusu dhamira ya Herodi na kwamba waondoke kwa kupitia njia nyingine.
“Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.” Mathayo 2:12
“Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.” Mathayo 2:13
13. MKEWE Pilato;
Akiwa katika kutaka kutoa hukumu juu ya Yesu wa Nazareth, Pilato mkewe alimjia na kumuonya kutokunyoosha mkono wake juu ya Yesu kwasababu anakiri kupatabsana tabu usiku katika ndoto ya kwamba huyu Yesu kwamba ni mtu wa Haki na wala hana hatia. Nadhani utakumbuka ni Pilato ndiye aliyesema “mimi sioni hatia juu ya mtu huyu, nimenawa mikono yangu na damu yake isiwe juu yangu na nyumba yangu.”
“Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.” Mathayo 27:19
Tofauti Ya Ndoto Na Maono:
Zipo namna tatu za kuingia katika ulimwengu wa ROHO. Namna hizo ni kwa NDOTO na MAONO na MAOMBI. Kwa maana hiyo NDOTO na MAONO zote ni njia za kuingia katika ulimwengu wa ROHO. Lakini pia NDOTO ni ufunuo wa picha na matukio; ilhali MAONO pia.
Tofauti yao inakuja kwamba MAONO humpata mtu akiwa macho kabisa, ubongo wake ukiwa active wakati NDOTO inamtokea mtu akiwa katika usingizi mzito sana, mwili umepumzika na ubongo unafanya kazi.
Ukisoma Biblia utakuta karibu maeneo yote; ndoto na maono yametumiwa kwa namna moja. Unaweza kukuta ndoto inaitwa maono ama maono yakaitwa ndoto. Lakini pia haijaathiri maana halisi ya tofauti zao.
Sunday, April 17, 2022
Je, ni halili mkristo kuolewa ao kumuoa muislamu?
Jibu langu ni "Hapana", Lakini natumai utasoma vizuri maelezo yangu hapo chini ili kuelewa ni kwa nini nimesema "hapana".
»Itakuwa vyema tukitumia bibliĆ kufahamu mkristo ni nani na muislamu ni nani.
»MKRISTO ni mtu aliyeokoka kwa kuamini kufa na kufufuka kwa Kristo na anamfuata Bwana Yesu. Tunaliona hili katika kitabu cha WARUMI 10:9 " Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua katika wafu; utaokoka".
»Tunapomuita Yesu kuwa ni Bwana yaani Bwana Yesu, tunamaanisha kuwa yeye ni kiongozi au mtawala wa maisha yetu tukifanya yote ayatakayo (MATHAYO 7:21).
»Kwa hiyo Mkristo hujibidisha kumpendeza Mungu, hata kama kuna muda ataonekana kushindwa(kuchelewa kuolewa), hapaswi kumkana Yesu. Kama ataziacha amri za Mungu, hatoweza kuingia katika ufalme wa Mungu pamoja na kwamba hapa duniani alijiita kuwa yeye ni Mkristo.
MUISLAMU NI NANI?
»Pamoja na maandiko mengi ya kiislamu kutakakufanana na ya Kikristo(kwa sababu walinakili), lakini imani ni tofauti na tofauti zake ni nyingi mno ukizichunguza kwa makini.
»Waislamu huamini Yesu kuwa ni nabii, hawaamini kuwa Yesu ni Mungu, wala hawaamini kuwa Yesu alifufuka. Hii ndio sababu ya Wakristo na Waislamu kutokuwa sambamba, kwa sababu wanaamini vitu tofauti kuhusu kiungo muhimu katika Ukristo yaani Yesu (WARUMI 10:9).
»Katika YOHANA 3:18 tunaona kuhusu Yesu " Amwaminiye yeye(Yesu) hahukumiwi(hana hatia); asiyemwamini(Yesu) amekwisha kuhukumiwa(ni mwenye hatia); kwa sababu hakuliamini jina pekee la mwana wa Mungu".
»Muislamu ni mwenye hatia, aliyehukumiwa tayari kwa sababu hamwamini Yesu.
»Tukisoma katika 2 WAKORINTHO 6:14-17 "Msifungiwe nira pamoja na wasioamini........yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?......." Mkristo hapaswi kuolewa na muislamu.
»Hata kama mwanamke(mkristo) amefiwa na mume yaani ni mjane, anaruhusiwa kuolewa na mtu yeyote amtakaye katika Bwana tu. 1 WAKORINTHO 7:39 " ....yu huru kuolewa na mtu yeyote amtakaye; katika Bwana tu".
»Hii ni amri ya Mungu na ni hekima pia, kwa sababu Mungu anatuambia mahusiano ya ndoa ni moja ya mambo yanayotusaidia kukua(kuimarika) kiroho na kuwa na nguvu za Kimungu na hayapaswi kutuzuia kukua kirohi.
»Kwa hiyo basi, wanamume wameamriwa kuwapenda wake zao na kuwafanya kuwa watakatifu(WAEFESO 5:25-33). Je, mwanamume wa kiislamu anaweza kufanya hivi hali yeye mwenyewe hamwamini Yesu? Jibu ni hapana hawezi badala yake ni kukuangusha kiroho na kukufanya uigeukie miungu ya kigeni ambayo ni chukizo kwa Mungu wetu.
»Tafuta kuwa karibu na Mungu, usikate tamaa kwa kuona umri umeenda wala huolewi; mwombe Mungu naye atakupa kwa wakati wake tena aonao kuwa wafaa.
»Je, unamfuata Yesu au unamwita Bwana, Bwana hali huyatendi yale asemayo? Je, unahakika kuwa ukifa unaingia mbinguni?
Jifunze kuusu Pasaka
»Neno "Pasaka" linatokana na neno la kiebrania "PESACH" kwa kiingereza ni lenye maana "PASS OVER" yaani "KUPITA JUU YA".
»Mwanzo wa Pasaka ulikuwa ni wakati wa nabii Musa (KUTOKA 12:14,17-18,21, KUTOKA 13:3-4; HESABU 9:21-30).
»Pasaka ni tendo la Bwana kupita juu ya nyumba za wana wa Israeli huko Misri, pale alipoiona damu ya mwanakondoo wa Pasaka katika vizingiti vya juu na miimo miwili ya milango yao alipita juu na kuacha kuwaharibu. Walioharibiwa walikuwa ni Wamisri ambao alama ya damu haikuonekana katika nyumba zao (KUTOKA 12:21-30).
»Mungu aliwaagiza wana wa Israeli kuikumbuka siku hii.
»Siku kuu hii ya Pasaka ilifanyika kuwa kumbukumbu kila mwaka katika mwezi wa Kiyahudi unaoitwa " NISAN" (NEHEMIA 2:1) au "ABIB" (KUTOKA 13:3-4). Siku kuu hii ilifanyikwa kwa juma moja yaani siku ya 14 hadi siku ya 21.(KUTOKA 12:14,17-18; HESABU 9:1-5).
»Mwezi wa "NISAN" au "ABIB" katika kalenda yetu ni kati ya mwezi "MARCHI" na "APRILI". Kuanza kwa mwezi ABIB kunategemeanana mwandamo wa mwezi . Ndiyo maana tarehe za siku kuu ya Pasaka hubadilika kila mwaka, Lakini huwa ni kati ya mwezi Marchi na Aprili.
»Katika kusherekea siku kuu hii walihitajika kuchinja wanyama wengi sana ili kupata damu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kama ondoleo la dhambi. Kwa wastani katika kipindi cha Pasaka walichinjwa wanyama 256,500 (laki mbili hamsini na sita elfu na mia tano).
»Katika kusherehekea Pasaka, Wayahudi walifanya mkutano mkubwa au konferensi ambapo walikusanyika pamoja na kula na kunywa na kuwa na muda mrefu wa kulisikia Neno la Mungu.
»Siku kuu hii iliendelea hadi katika kipindi cha Yesu Kristo. Yesu kristo mwenyewe alikuwa akienda kusherekea Pasaka(LUKA 2:41-52; YOHANA 2:13,23).
»Hiki kilikuwa ni kivuli cha Yesu Kristo kama mwanakondoo wa Pasaka aliyechinjwa msalabani.
»Yesu kristo alitolewa kusulubishwa wakati wa pasaka kama Pasaka wetu(YOHANA 18:39, 19:14-18; 1 WAKORINTHO 5:7). Kwa sababu hiyo, sasa hatuna haja ya kuchinja wanyamatena kama sadaka bali ni kumwamini Yesu ambaye ndiye sadaka yetu.
»Kila amwaminiye Yesu Kristo kwa Imani tu, damu ya Yesu hunyunyizwa juu yake na kuoshwa dhambi zote na kuwa salama(1 PETRO 1:2). Sasa hakuna haja tena ya kuchinja wanyama.Sasa tunaingia patakatifu pa Bwana(hekaluni) kwa damu ya Yesu(WAEBRANIA 10:19). Shetani ni Mharibu lakini hawezi kumharibu yeyote aliyenyunyiziwa damu ya Mwanakondoo (1 PETRO 1:2; UFUNUO 12:11).
»Kila asiyemwamini Yesu ghadhabu ya Mungu inamkalia, amekwisha hukumiwa (YOHANA 3:3,16-18). Kwa jinsi hiyo basi, ni busara mtu kusherehekea Pasaka pale tu ambapo amekwisha nyunyiziwa damu ya Yesu na kumshinda Shetani. Kinyume cha hapo, ni kufanya mchezo wa kuigiza(YOHANA 1:35-36, 10:10).